Mwigizaji maarufu wa Bongo Movie hapa nchini Ray Kigosi amesema kwamba
yeye hajawahi kujichubua bali huwa anakunywa maji mengi pamoja na
kufanya mazoezi .
Ray ameyasema hayo wakati akifanya mahojiano katika kipindi cha ENews
kinachorushwa na EATV na kusema kwamba hua anakwenda salon mara moja kwa
wiki kwa ajili ya kusafisha uso wake (Scrub) ili akiwa anafanya kazi
zake watu waweze kumwona vizuri na kupenda kazi zake.
Naye Mpenzi wake Chuchu Hans amesema kwamba Mpenzi wake hajichubui bali
ni maisha yamemkubali tofauti na hapo nyuma alivyokuwa anahangaika
kuinua sanaa na kipaji chake.
Katika kipengele cha ''Cheche'' ambacho majirani hupewa nafasi ya
kumzungumzia msanii au mgeni wa siku kwenye show wamesema kwamba Ray
apunguze kutumia vipodozi kwani anakuwa kama mchina.
Pia wamemtaka mwigizaji huyo kuwa na moyo wa kusaidia wasanii chipukizi ilikukuza tasnia ya uigizaji hapa nchini.
0 comments:
Post a Comment