Top Ad 728x90

Friday 19 February 2016

Peter wa P Square Aomba Radhi kwa Kuweka Mgogoro wa Kifamilia Mtandaoni?


Msanii peter ambaye anaunda kundi la P Square, ameomba radhi kwa kitendo chake alichokifanya, ingawa hajaweka bayana analenga lipi katika aliyoyafanya kwenye kundi lake abalo ni la familia, na jamii kiujumla.

Kwenye ukurasa wake wa twitter Peter ameomba msamaha huo akiandika maneno haya..... "I am not perfect i make mistakes, and it hurts people. But when I say sorry I mean it. I am so SORRY for my actions. I sincerely apologize", aliandika Peter akimaanisha kwamba (Mimi siko sahihi nafanya makosa, na inawaumiza watu, lakini ninaposema samahani namaanisha, samahani sana kwa vitendo vyangu, naomba msamaha huu kwa dhati).

Hapo jana kuliiibuka mzozo mkubwa kati ya kundi hilo ambapo Peter akitaka kaka yao Jude ambaye ndio kiongozi wao atoke kwenye kundi na kuwaacha yeye na Paul, kitendo ambacho pacha wake Paul alikijia juu na kumwambia kama ni matatizo ya familia ni ya kuzungumza nyumbani, na sio kwenye mitandao.

0 comments:

Post a Comment

Top Ad 728x90