Top Ad 728x90

Wednesday 24 February 2016

Baada ya Lundenga Kukemea Matusi ya Mange, Wizara ya Mambo ya Ndani na Jeshi la Polisi Latoa Onyo


Wiki iliyopita kupitia mtandao wa Instagram,Blogger Mange Kimambi alimshambulia kwa matusi Aliyekuwa Miss Tanzania Hoyce Temu kwa kisa ambacho hata hakihusiani nae.Vilevile katika kashfa na tuhuma hizo walihusishwa hata watu wasiohusika katika ugomvi wa Mange na Ndugu yake Hoyce kinyume na sheria.

Hoyce Temu alieleza kusikitishwa kwake na maneno ya kashfa yasiyokuwa na chembe ya ukweli yaliyoelekezwa kwake na blogger huyo

Wadau mbalimbali walitoa maoni yao akiwepo Mratibu wa Miss Tanzania Hashim Lundenga aliyelaani vikali tabia hiyo iliyofanywa na Blogger huyo kuchafua majina ya watu kwa kashfa na tuhuma za uongo kwa malengo yasiyoeleweka.

Alisema inasikitisha kuona mtu ambaye anaisaidia jamii kwa hali na mali akitungiwa kashfa za uongo na kuchafuliwa jina pasipo sababu yoyote ya msingi.

Vilevile waziri wa mambo ya ndani ameonya kuwa Jeshi la polisi litachukua hatua kali bila huruma na bila kujali mhusika alipo kwa wale wote wanaotumia mitandao ya kijamii vibaya huku msemaji wa jeshi hilo akitoa msimamo mkali dhidi ya wale wote wanaotumia mitandao vibaya.

Amewataka wote ambao wanachafuliwa kwa njia ya mitandao waripoti TCRA au jeshi la polisi kwa hatua kali bila kujali jiografia ya makazi ya wahusika au mipaka.

0 comments:

Post a Comment

Top Ad 728x90