Top Ad 728x90

Sunday 28 February 2016

Mwili wa Marehemu Uliyozikwa Kikristu Wazua Zogo Waislam Waandamana Wakitaka Kuufukua Mwili Uzikwe Kiislam


KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida waumini wa dini ya kiislamu pamoja na viongozi wa dini hiyo wilaya na mkoa wa Geita, wameandamana mpaka kwenye familia ya marehemu Samweli Malugala  wakitaka kufukua mwili wake uliozikwa kikristu na ndugu zake.

Sakata hilo limekuja siku moja baada ya kuzikwa nyumbani kwao katika mtaa wa Mkolani kata ya Nyankumbu mjini Geita, ambapo viongozi wa dini ya Kiislamu walifika nyumbani kwa marehemu kutoa zuio la kuzikwa, na kwa vile hawakuwa na vigezo hawakuweza kufanikiwa kusudio lao.

Jana majira ya saa sita mchana Waislamu wakiwa wameongozana na maimamu wa msikiti wa ijumaa mjini Geita pamoja na mwenyekiti wa bakwata Mtaa wa Kalangalala walifika mpaka kwenye familia ya marehemu Samweli na hapa na kuanza kuongea kilichowapeleka.

Naye mwanafamilia Lucas Paul ambaye ni mtemi wa sungusungu Mtaa wa Mkolani , amewataka wafuate taratibu ya kufanya zoezi lao wakiwa chini ya uongozi wa Mtaa au Kata.

Muda mfupi baada ya malumbano hayo, mkuu wa polisi wilaya ya Geita  Ali kitumbo amefika katika enao hilo la tukio  na kuwataka Waislamu wafuate taratibu na kwamba wao polisi  wako tayari kusimamia zoezi hilo.

Pamoja na kwamba marehemu amekwisha zikwa kikristu kesi ya msingi itaanza kusikilzwa tarehe moja mwezi machi mwaka huu katika mahakama ya wilaya ya Geita, ambapo itaamua nani ana uhalali wa kuuzika mwili huo.

0 comments:

Post a Comment

Top Ad 728x90