Top Ad 728x90

Sunday 28 February 2016

Dudu Baya Awaka Baada ya Kuambiwa ni ‘Baba wa Nyumbani’ Hana Cha Kufanya

Mashakibi wa muziki wamemtibua Dudu Baya baada ya kumwambia amekosa cha kufanya ndio maana amekuwa akiwatukana wasanii wenzake ovyo.

Rapa huyo ambaye ameachia wimbo ‘Kokoriko’ hivi karibuni, ameiambia Bongo5 kuwa mashabiki wanashindwa kujua kuna vitu gani nyuma ya pazia ya maisha ya wasanii.

“Kuna mashabiki nimewaona Enewz ya EATV wanasema nimekosa cha kufanya ndio maana nakaa tu nyumbani, nataka wajue muziki sio mkojo ukijisikia tu unautoa mashabiki wajue, mpaka kazi inatoka wajue kuna kazi kubwa imefanyika” alisema Dudu Baya.

Aliongeza,
“Mimi bado ni mfanyabiashara, Je kampuni ya Mambaz Timber ni yao?. Je kampuni ya Mambaz Entertaiment ni yao?. Kama ni mamluki wajipange, mimi ni Mamba na wasione nipo kimya katika muziki wakadhani sina cha kufanya.Kukaa maskani ni sehemu ya maisha yangu na sitaacha na si kila mtu na sio lazima ajue shughuli zangu zingine,”

0 comments:

Post a Comment

Top Ad 728x90