Tuesday, 1 March 2016
by Mng'atuzi blog
00:12
Mwambigija na viongozi wengine akiwamo katibu wa chama wilaya, katibu mwenezi na wajumbe wengine wa kamati ya utendaji wilaya, walivuliwa nyadhifa zao hivi karibuni baada ya kumalizika kwa kikao kilichofanyika usiku chini ya uongozi wa Makamu Mwenyekiti wa Chadema Taifa Zanzibar, Issa Said Mohamed.
Akizungumzia kuvuliwa uongozi, Mjumbe wa Mkutano Mkuu, Hezron Mwaisengela ambaye pia ni Katibu Kata ya Mwakibete, alisema hawakubaliani na uamuzi wa kuivua madaraka kamati ya utendaji kwa kuwa hawakushirikishwa. “Kilichofanyika hakikubaliki na ni uvunjaji wa Katiba ya chama na tukiendelea kulea upuuzi huu, tutavurugana kabisa.
“Viongozi hao walichaguliwa na wajumbe wa mkutano mkuu ambao ni sisi na hata kuondolewa kwa namna yoyote ile ni lazima uitishwe mkutano mkuu kinyume na hapo sisi tunaendelea kuwatambua viongozi hawa,” alisema Mwaisengela.
Mjumbe mwingine, Frank Mwankina ambaye ni Mwenyekiti wa Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha) Kata ya Nzovwe, alisema wapo kwa ajili ya kulinda masilahi ya chama na siyo vinginevyo.
“Kama kuna ukweli wowote kuhusiana na tuhuma hizo walipaswa kujadiliwa kwenye vikao rasmi,” alisema Mwankina.
Alisema Mbowe aliyefika hivi karibuni mkoani humo kusikiliza mgogoro huo, alipokea malalamiko ya kila upande, lakini hawakupaswa kuwavua madaraka ambayo waliyapata kwa kuchaguliwa.
Kauli za wajumbe hao zinatolewa wakati hali ya Chadema jijini hapa ikizidi kuwa tete kutokana na madiwani kuhasimiana
by Mng'atuzi blog
00:12
Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mwantumu Mahiza amesema Sh36 bilioni zilizotengwa
kwa ajili ya kutekeleza miradi 66 ya ujenzi wa mabwawa ya umwagiliaji
Tanga, zimefujwa.Mahiza alisema hayo juzi katika kikao cha wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama, makandarasi, wahandisi na wakurugenzi wa wilaya za Mkoa wa Tanga.
Alisema ni miradi 30 tu iliyotekelezwa huku mingine 36 ikiwa haijatekelezwa na fedha kutumika.
Mahiza alifanya kikao hicho baada ya kumaliza ziara yake ya siku 10 ya kukagua miradi ya maji mkoani humo na kubaini ufisadi huo.
“Nawapa siku 14 mniletee maelezo kwa nini msichukuliwe hatua kwa kufanya kazi isiyo na tija na kuonyesha uchu wa kutaka fedha za miradi hali mkijua hamuwezi kuitekeleza na kutoishauri Serikali kuhusu njia sahihi,” alisema.
Alisema makandarasi na wahandisi ambao hawakutekeleza miradi watakuwa chini ya uchunguzi wa maofisa wa Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (Takukuru), Idara ya Usalama wa Taifa na Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).
“Sh36 bilioni zimehujumiwa na wataalamu (watendaji) ambao hawaitakii mema Tanga, imenigusa, imeniumiza kupita kiasi, nimekasirika, haya ni majipu makubwa tutayatumbua bila ganzi.
“Mmetutengenezea fitina kati ya Serikali na wananchi,” alisema Mahiza.
Alisema baada ya kupokea maelezo hayo atakutana na kamati yake ya ulinzi na usalama kushauriana kisha majina yote ya waliohusika yatafikishwa kwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kwa ajili ya uamuzi.
Mhandisi wa Maji Mkoa wa Tanga, Ephraim Minde alisema miradi hiyo 30 iliyokamilika ipo katika Wilaya za Korogwe, Lushoto, Kilindi na Tanga.
Mmoja wa wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Noel James alisema mradi wa umwagiliaji wa Mwakijembe Wilaya ya Mkinga unaofadhiliwa na Benki ya Dunia.
by Mng'atuzi blog
00:09
Uchaguzi huo ulipangwa kufanyika Januari 23, mwaka huu, lakini uliahirishwa ili kuandaa mfumo bora wa upatikanaji wajumbe kutokana na CCM kutaka kuingiza wapigakura nje ya waliotakiwa.
Ulikwama tena Februari 8, baada ya Halmashauri ya Jiji la Dar kubaini kasoro ya nyongeza ya majina 14 ya wajumbe kutoka manispaa za Ilala na Kinondoni.
Jumapili iliyopita ilikuwa ni mara ya tatu, kukwama tena kutokana na zuio lililosababishwa na kesi iliyofungiliwa na Saad Kimji na Suzan Masawe.
Hata hivyo, zuio hilo la muda la Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu lililotumika kuahirisha uchaguzi wa meya na naibu meya wa Jiji, uliopaswa kufanyika Februari 27, 2016 limebainika kuwa ni batili.
Jana, Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Kisutu, Waliarwande Lema alisema Saad Kimji na Suzan Massawe walifungua kesi Februari 5, 2016 wakizuia uchaguzi wa meya na naibu wake ambao ulipaswa kufanyika Februari 8,2016.
Hakimu Lema alibainisha baada ya kufungua shauri hilo, Mahakama ya Kisutu iliweka zuio la muda ili kesi hiyo ianze kusikilizwa Februari 15, 2016 lakini walalamikaji hawakutokea mahakamani hivyo mahakama ikapanga kusikiliza kesi hiyo Februari 23, lakini hawakutokea pia.
Alisema kutokana na hali hiyo, aliliondoa shauri hilo mahakamani hapo na hivyo zuio hilo likawa limekufa.
Aliongeza kuwa aliyesema Mahakama ya Kisutu imetoa zuio ni muongo na kwamba zuio halali ni lazima liwe na jina la Hakimu pamoja na sahihi.
Kukamatwa kwa Mdee
Katika sakata la jana, Mdee na madiwani wengine watatu walilazwa rumande kutokana na kutuhumiwa kumshambulia Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es Salaam, Theresia Mmbando
Wanatuhumiwa kufanya kosa hilo baada ya vuta nikuvute kutokea Jumapili iliyopita wakati shughuli ya kuwasaka viongozi hao wa jiji zilipokwaa kisiki kwa mara ya tatu, na CCM kuamua kukimbilia mahakamani.
Hali hiyo, ilizua tafrani kati ya madiwani na wananchama wa vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) baada ya uchaguzi huo kuahirishwa kwa zuio la muda la Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.
Tafrani hiyo ndiyo iliyosababisha vurugu ambazo inadaiwa kuwa katika purukushani hizo Mdee alimshambulia Mmbando mara baada ya kutangaza kuahirisha uchaguzi huo.
Polisi waliokuwa wanalinda usalama kwenye ukumbi wa Karimjee ambako uchaguzi huo ulitakiwa kufanyika, walimtoa nje Mmbando.
Akitoa maelezo mafupi kwa waandishi wa habari jana baada ya Mdee kuhojiwa kwa takriban saa sita, wakili wake , Profesa Abdalah Safari alisema mbunge huyo anashikiliwa kwa kosa hilo na atalala rumande.
“Kimsingi nilikuja kumsikiliza akitoa maelezo yake, ameshatoa lakini hakuna ushahidi wowote wa kosa analodaiwa kufanya la kushambulia Theresia,” alisema.
Hata hiyo, Profesa Safari alisema kutokana na kosa hilo Mdee alikuwa na haki ya kuwekewa dhamana lakini polisi wamekataa.
“Mdee angeweza kujidhamini hata mwenyewe lakini wamekataa na kutokana na kosa hili anatakiwa kulala rumande kwa saa 48, zikizidi ina maana atapelekwa mahakamani,” alisema.
Profesa Safari, ambaye pia ni makamu mwenyekiti wa Chadema Bara, alisema mbali na Mdee pia madiwani watatu wanashikiliwa na polisi kwa kosa hilo.
Madiwani hao ni Humphrey Sambo wa kata ya Mbezi, Ephraim Kinyafu (Saranga), wakati hakumtaja jina diwani wa tatu.
Awali wakati mahojiano hayo yalipoanza saa 7:00 mchana, taarifa kutoka kwa mmoja wa makada wa chama hicho zilieleza kuwa Mbunge wa Ukonga (Chadema), Mwita Waitara pia alitakiwa kufika kituoni hapo kutoa maelezo na anatarajiwa kuwasili leo.
Wakati wa polisi wakimhoji Mdee, wanachama wa Chadema walifika kituoni hapo, akiwapo Ester Bulaya, ambaye ni mbunge wa Bunda Mjini, Esther Matiko (Bunga Vijijini) na Henry Kilewo ambaye ni kanda wa Chadema.
Mapema jana mchana kabla ya Mdee kufikishwa kituoni hapo, ilielezwa kuwa polisi walizingira nyumba yake na kumtaka aende kituoni.
Hata hivyo, mbunge huyo hakutoka hadi alipowasiliana na wakili wake ambaye alienda naye kituoni kwa ajili ya mahojiano.
by Mng'atuzi blog
00:08

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), January Makamba ametofautisha nyakati za utawala wa Serikali ya Awamu ya Nne iliyoongozwa na Dk. Jakaya Kikwete na zilizopita na huu wa Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais John Magufuli, huku akiitoa kasoro iliyopita.
Makamba ameeleza kuwa wakati tawala zilizopita, watu walikuwa wakionewa haya na na kujuana kulichukua nafasi tofauti na awamu hii inayochukua hatua stahiki bila kujali.
“Nadhani moja ya changamoto zilizosababisha huko nyuma tusifanikiwe sana katika suala la uwajibikaji, ni hili suala la kuoneana haya. Suala la kujuana kidogo na kusitiriana,” Makamba aliliambia Gazeti la Mwananchi hivi karibuni.
Alisema kuwa utamaduni huo unapoendelea na kuota mizizi, suala la uwajibikaji huwa kikwazo na hatua stahiki dhidi ya watu wanaofanya makosa hushindwa kuchukuliwa.
Makamba ambaye alikuwa Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia katika Serikali ya Awamu ya Nne, alieleza kuwa hatua za utumbuaji majipu zinazochukuliwa hivi sasa dhidi ya wakwepa kodi na watumishi wanaovunja sheria na kutowajibika ni sahihi na kwamba kama kuna mtu anaona anaonewa bado anayo nafasi ya kutafuta haki yake kwenye vyombo vya kisheria.
“Kikubwa tu ambacho mimi ninaamini ni kwamba kunahitajika kujenga utamaduni mpya wa watu kuogopa na kuheshimu wajibu wao, na kwamba hizi kazi si kazi zetu za kudumu. Wakati wote unapofanya makosa basi kuna Mamlaka ya kukuchukulia hatua,” alisema.
Makamba alisisitiza kuwa ni sahihi kuchukua hatua hivi sasa dhidi ya makosa yaliyofanyika katika utawala uliopita, “Kama huko nyuma hakukuwa na utashi wa mfumo wa kuwezesha makosa hayo kubainika, lakini utashi huo upo sasa, basi hatua zichukuliwe.”
by Mng'atuzi blog
00:07

Maafisa wa polisi na utawala wa mji mkuu wa Bujumbura Burundi wamegundua kaburi la halaiki linaloshukiwa kuwa na takriban miili 30.
Mwandishi wa BBC aliyeko huko Prime Ndikumagenge anasema kuwa miili 3 na fuvu la kichwa ilipatikana katika eneo la Mutakura Kaskazini mwa Bujumbura.
Kitongoji hicho cha Mutakura ni moja ya ile iliyosheheni wafuasi wa upinzani ambao walijitokeza mabarabarani wakiandamana kupinga kauli ya rais Pierre Nkurunziza kuwania muhula wa tatu uongozini.
Nkurunziza alitangaza nia ya kuwania muhula wa tatu mwezi Aprili mwaka uliopita kinyume cha katiba akidai kuwa mhula wa kwanza hakuchaguliwa na umma.
Wapinzani wake hata hivyo wanadai kuwa alikiuka katiba ya taifa.
Meya wa mji wa Bujumbura Freddy Mbonimpa anasema walipokea habari hiyo kutoka kwa ''wahuni waliojisalimisha kwa utawala''.
Haikuelezwa kwa hakika waliuawa lini au na nani na nani aliyewazika pahala hapo.
Meya huyo hata hivyo alidai kuwa waliopatikana wameuawa walikuwa ni wafuasi wa rais Nkurunziza.
Kuwepo kwa makaburi ya halaiki kuligunduliwa kwanza na kundi linalopigania haki za kibinadamu la Amnesty International mwezi Januari.
Ripoti hiyo ya kundi la kutetea haki za binadamu la lilichapishwa tarehe 11 Desemba mwaka uliopita siku moja baada ya serikali kukiri kuwa wamewaua watu 79 na kupoteza maafisa 8 wa polisi.
Meya huyo leo amekiri kuwa utawala wake ulizika miili ya watu 58 katika makaburi ya halaiki katika makaburi yanayofahamika.
Umoja wa Mataifa unasisitiza kuwa zaidi ya watu 430 waliuawa nchini Burundi tangu kauli ya rais Nkurunziza kubainika mwezi Aprili.
by Mng'atuzi blog
00:06
Hata hivyo, taarifa iliyotolewa na mahakama hiyo jana, ilieleza kuwa kesi hiyo namba 006/2015 iliyopangwa kusikilizwa Machi 11 haitasikilizwa katika mahakama ya wazi.
Ni kesi mbili pekee kati ya 50 zitakazosikilizwa kwenye mahakama ya wazi, ikiwamo inayomhusu mwanasiasa maarufu wa Rwanda, Victoire Ingabire aliyoifungua kupinga ukiukwaji wa haki anaofanyiwa na Serikali yake.
Pia, mahakama ilieleza kuwa kikao hicho cha 40 cha kawaida kitakamilika Machi 18 na kutoa uamuzi wa mashauri manne.
Kesi ya Ingabire inayotarajiwa kuvuta hisia za watu wengi ikizingatiwa upinzani ambao amekuwa akiuonyesha dhidi ya serikali yake, itasikilizwa Machi 4.
Katika kesi hiyo, Ingabire pamoja na mambo mengine anadai haki zake kuvunjwa ambazo zinatajwa kwenye Mkataba wa Mahakama hiyo Ibara ya 7, 10 na 18 hivyo anaitaka itoe uamuzi.
Pia, Taasisi ya Action Pour la Protection des Droits de I’Homme (APDH) inaishtaki Serikali ya Ivory Coast kuvunja mkataba wa Mahakama ya Afrika na Haki za Binadamu Ibara ya 3 na 17 katika kesi namba 001/2014, iliyopangwa kusikilizwa Machi 3.
Mahakama hiyo inaundwa na majaji 11 kutoka nchi wanachama wa Umoja wa Afrika (AU) na inakuwa na vikao vinne kwa mwaka, kufikia Januari 31 tayari ilikuwa imepokea kesi 74 kati ya hizo 25 imetolewa uamuzi.
Maombi manne yamepelekwa kwa uamuzi zaidi kwenye Kamisheni ya Afrika ya Haki za Binadamu.
Subscribe to:
Posts (Atom)










