Top Ad 728x90

Sunday 6 March 2016

Mange Kimambi Afunguka Baada ya Mtaliano Kuandika Barua ya Kuwashafisha January na Mwamvita Makamba....

by





"Mangekimambi_ hii ndio Tanzania yetu. Mlalamikaji ambae a few hrs before aliingia Twitter Na kumtishia January Kuwa atae expose na Safari Yao ya Dubai amesainishwa na barua na wana sheria kabisaa ya kumsafisha January Makamba! . .

Have you guys seen anything like this before?? Does it make sense?? a few hrs before mlalamikaji anatoa vitisho hadharani then anafanya a complete 100% turn around , akili kichwani kwako Mtanzania! Wow! Anyways, like I said any reasonable average person anaelewa what happened, you don't need to be a genius. Yani hata Waziri Mkuu na Rais wakiamua kumwacha January ni vile waamue but from zile audio za Mwamvita, to interview ya January hata wao wanajua January is guilty as charged!

Barua yenyewe wamemuandikisha fasta Mpaka wamekosea date

Hata wasipomchukulia hatua Ila In 2020 we will not forget , voice note bado zitakuwepo, email bado zitakuwepo, interview ya January bado itskuwepo Na tutawakumbusha Watanzania " Mange

Rais Magufuli Ampiga Chini Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue.....John Kijazi Kateuliwa Kuchukua Nafasi Yake

by


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli amemteua Balozi Mhandisi John William Kijazi kuwa Katibu Mkuu Kiongozi. 

Kabla ya uteuzi huo Mhandisi Kijazi alikuwa Balozi wa Tanzania nchini India. Kufuatia uteuzi huo, aliyekuwa Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue atapangiwa kazi nyingine.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi  wa Mawasiliano,
 IKULU-Dar es Salaam
06March,201
Katibu Mkuu Kiongozi Mpya, Balozi John William Kijazi

Ushindi wa Lulu na Richie kwenye AMVCA 2016 utaziongezea pumzi filamu za Kibongo

by
Tuzo za Africa Magic Viewers Choice Awards, ni sawa na Oscars za Afrika. Ndiyo tuzo kubwa zaidi zinazoikutanisha tasnia ya filamu Afrika nzima pamoja.

Utofauti kati ya tuzo za Oscars na AMVCA ni kuwa tuzo za Oscar zinaikutanisha industry ya filamu ya Marekani iliyounganika pamoja, Hollywood bali AMVCA ni tuzo zinazokutanisha industry ndogo ndogo za nchi za Afrika.

Na kwa kiasi kikubwa tuzo za AMVCA ambazo mwaka huu zimetolewa kwa mwaka wa nne zimetawaliwa na Nollywood na kwa mbali tasnia ya filamu ya Afrika Kusini. Kwa kuona hivyo, waandaji walitengeneza tuzo za kikanda na za lugha maalum. Ndiyo maana kuna tuzo ya filamu ya Kiswahili na ya Afrika Mashariki.

Kwa mwaka huu tuzo hizo zote zimekuja Tanzania, ambapo Single Mtambalike maarufu kama Richie ameshinda kipengele cha filamu ya Kiswahili kupitia Kitendawili. Elizabeth ‘Lulu’ Michael alishinda kipengele cha filamu bora ya Afrika Mashariki, kupitia Mapenzi.

Na tumeshuhudia wenyewe kuwa ushindi huu umeshangiliwa zaidi na kurejesha imani katika filamu zetu. Ushindi wa Lulu na Richie unatupa moyo wa kuamini katika kazi za wasanii wetu. Ushindi huu umekuja katika kipindi ambacho tasnia ya filamu ya Tanzania imeshuka kwa kiasi kikubwa katika pande nyingi. Imeshuka kwenye mauzo na usambazaji kiasi ambacho wasambazaji wakubwa wamepunguza kasi ya kusambaza kazi kama zamani na kuwafanya waigizaji wengi kubaki na filamu zao mkononi wasijue namna ya kuzisambaza.

Ni kwasababu ni watanzania wachache wenye muamko wa kutoa fedha mfukoni na kununua filamu za nyumbani. Pengine kwasababu ya utandawazi ambapo tumekuwa ‘exposed’ na filamu bora kutoka Hollywood, imekuwa ngumu sana kuziamini filamu za nyumbani hasa tunapotaka kuzifananisha. Kuna sababu nyingi sana zinazochangia tuziweze kufikia hata asilimia 10 ya ubora wa filamu za wenzetu. Uchumi, teknolojia, ujuzi, elimu, utafutaji na unolewaji wa vipaji kwenye filamu na mambo mengine kibao yanaifanya tasnia yetu iendelee kudoda.

Lakini pengine kama tukiamua kuweka nguvu kwenye vitu vinavyowezekana kama vile kutengeneza filamu zenye story nzuri na zilizobeba uhalisia pamoja na uchaguzi mzuri wa wahusika watakaowasilisha maudhui kwa ufahasa, watanzania wanaweza kushawishika kuzinunua filamu za nyumbani. Inabidi filamu zianze kutengeneza mjadala kama ambavyo muziki wa Bongo Flava umefanikiwa. Kwamba Ray akitoa filamu yake, watu waijadili kwenye mitandao ya kijamii kama ambavyo Diamond au Alikiba na wasanii wengine wakiachia video zao.

Tukirudi kwenye ushindi wa Lulu na Richie kwenye AMVCA, naamini kuwa umepeleka ujumbe Afrika kuwa Tanzania ina kitu. Kama ambavyo kimuziki tunaonekana kuwa vizuri, ni kwa kushinda tuzo kama hizi kunawashtua watu wa pande zingine za Afrika kuwa kumbe nasi tumo.

Cha msingi ni wasanii wetu kuongeza spidi zaidi kwa kutengeneza filamu ambazo hata kama zitatajwa kuwania tuzo hizo, zisiishie tu kuwekwa kwenye vipengele maalum, bali pia kwenye vipengele vya jumla. Tunapenda kuona siku moja Lulu, Kajala, Wema Sepetu, Nisha au Shamsa Ford wanashindana kwenye tuzo moja na Genevieve Nnaji wa Nigeria au Yvonne Nelson wa Ghana.

Tunapenda kuona siku moja Ray, Richie, JB au Hemedy wanashindana kwenye tuzo moja na Ramsey Noah wa Nigeria au Van Vicker wa Ghana.

Mimi ninaamini kuwa ushindi wa Lulu na Richie kwenye AMVCA 2016 utaziongezea pumzi filamu za Kibongo

Wema, Kajala Acheni Utoto Bwana!

by


KWENU warembo wa Bongo Movies, Wema Sepetu ‘Madam’ na Kajala Masanja. Habari zenu binafsi? Bila shaka ni wazima wa afya na mnaendelea na majukumu yenu ya kila siku. Kitambo kidogo sijawaona lakini naamini pumzi ya bure mnaendelea kuivuta ndiyo maana nasikia matukio yenu kwenye vyombo vya habari.

Mkitaka kujua afya yangu, mimi ni mzima. Namshukuru Mungu naendelea na shughuli zangu kama kawaida. Mungu ni mwema sana, anaendelea kubariki kazi ya mikono yangu, namuomba yeye aendelee kunibariki zaidi na zaidi.

Dhumuni la kuwaandikia barua hii ni kutaka kuwakumbusha kwamba nyinyi kwa sasa ni watu wazima. Umri wenu unatosha kabisa kusema haufanani na yale matukio yasiyokuwa na kichwa wala miguu. Mara kadhaa nimewahi kuwaambia, hata yale mashindano yenu ya kumwaga fedha ukumbini, nyakati hizi si zake.

Mambo ya kuibiana mabwana kama yalishatokea, itoshe sasa kusema ulikuwa ni ujana. Kwa kuwa ilitokea, hakuna namna zaidi ya kuyasahau na kuchapakazi. Soko lenu la filamu bado haliridhishi, lakini mnapaswa kukomaa ili angalau mtengeneze fedha kupitia kazi zenu na si kuhongwa.

Binafsi sikufurahishwa na tukio lenu la kukutana ukumbini na kuzinguana mbele ya kadamnasi lililoripotiwa wiki iliyopita na magazeti Pendwa. Lilikuwa tukio linaloonesha kwamba bado hamjakua kitu ambacho sitaki kukiamini.

Kama nilivyotangulia kusema hapo awali, huu siyo wakati wa nyinyi kuoneshana ubabe wa fedha. Kwamba eti kwa kuwa mwenzako kaenda kutunza msanii jukwaani, na wewe lazima utunze nyingi zaidi ili uonekane wewe ni zaidi.

Ndugu zangu, bahati nzuri maisha  yetu tunajuana. Kwa kiasi kikubwa natambua maisha ya wasanii wetu nchini hususan warembo. Wengi wenu hamtegemei sanaa kuendesha maisha yenu. Wengi mnategemea  mapedeshee au ‘mabwana’ kutamba mjini.

Niwashauri hizo fedha mnazozipata ni bora mngewekeza kwenye sanaa yenu. Mkajizatiti vizuri ili ziweze kuzaliana. Mnapigana ili iweje? Mnatambiana mbele za watu inawasaidia nini. Wenzenu wanapigana siku hizi wanaingiza fedha.

Nyinyi kazi yenu si ubondia. Kazi yenu ni uigizaji. Igizeni kwelikweli na Watanzania wawaunge mkono kwa kununua kazi zenu. Sanaa yenu ina changamoto nyingi, mnawezaje kuzishughulikia ikiwa hamna umoja.

Mtawezaje kutatua changamoto hizo ikiwa hamna upendo kati yenu? Si rahisi kutatua changamoto hizo wakati mna chuki. Ili mfanikiwe, mnahitaji kushirikiana. Shirikianeni ili muweze kuisogeza sanaa mbele, acheni vita ya kipuuzi mnayoendelea kuifanya.

Mkizingatia hayo niliyowaambia, hakika tutaona mabadiliko kwenu na sanaa kwa ujumla. Nina imani nyinyi ni watu wazima na mtajipanga upya na mtaanza kuchapa kazi kama kauli mbiu ya rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Joseph Magufuli, ‘Hapa Kazi Tu’.

Ni mimi mtu wenu,

Erick Evarist.

GPL

Mbwana Samatta Aonja Machungu Kwa Mara ya Kwanza Kwenye Timu yake Mpya ya Genk..

by


Nyota wa Tanzania Mbwana Samatta na klabu yake ya Genk walitoka vichwa chini baada ya timu yao kuchapwa bao 2-1 na klabu ya Standard Liege kwenye mchezo wa ligi kuu ya Belgium uliochezwa usiku wa Jumamosi March 5.

Genk wakiwa ugenini ndiyo walikuwa wa kwanza kupata bao dakika ya 42 kipindi cha kwanza likifungwa na Nikolaos Karelis na kuipeleka Genk mapumziko ikiwa kifua mbele kwa bao 1-0.

Dakika tatu baada ya kipindi cha pili kuanza, Ivan Santini akaisawazishia Standard Liege kabla ya Jean-Luc Diarra Dompe kuifungia Standard bao la ushindi na kupeleka msiba kwa Genk.

Kama kawaida Samatta iliingia uwanjani dakika ya 81 kuchukua nafasi Karelis lakini bado haikutosha kubalili matokeo.

Samatta anaishuhudia klabu yake ya Genk ikipoteza kwa mara ya kwanza tangu ajiunge nayo mwezi January akitokea klabu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemrasia Kongo.

Tuesday 1 March 2016

Mpasuko Chadema..Wamtaka Freeman Mbowe Akanusuru Jahazi Mbeya Mjini...

by

Siku chache baada ya Mwenyekiti wa Chadema Wilaya ya Mbeya Mjini, John Mwambigija na kamati yake ya utendaji kuvuliwa madaraka kutokana na msuguano baina yao, wajumbe wa mkutano Mkuu wa chama hicho wamemtaka Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe kuingilia kati mgogoro huo.

Mwambigija na viongozi wengine akiwamo katibu wa chama wilaya, katibu mwenezi na wajumbe wengine wa kamati ya utendaji wilaya, walivuliwa nyadhifa zao hivi karibuni baada ya kumalizika kwa kikao kilichofanyika usiku chini ya uongozi wa Makamu Mwenyekiti wa Chadema Taifa Zanzibar, Issa Said Mohamed.

Akizungumzia kuvuliwa uongozi, Mjumbe wa Mkutano Mkuu, Hezron Mwaisengela ambaye pia ni Katibu Kata ya Mwakibete, alisema hawakubaliani na uamuzi wa kuivua madaraka kamati ya utendaji kwa kuwa hawakushirikishwa. “Kilichofanyika hakikubaliki na ni uvunjaji wa Katiba ya chama na tukiendelea kulea upuuzi huu, tutavurugana kabisa.

“Viongozi hao walichaguliwa na wajumbe wa mkutano mkuu ambao ni sisi na hata kuondolewa kwa namna yoyote ile ni lazima uitishwe mkutano mkuu kinyume na hapo sisi tunaendelea kuwatambua viongozi hawa,” alisema Mwaisengela.

Mjumbe mwingine, Frank Mwankina ambaye ni Mwenyekiti wa Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha) Kata ya Nzovwe, alisema wapo kwa ajili ya kulinda masilahi ya chama na siyo vinginevyo.

“Kama kuna ukweli wowote kuhusiana na tuhuma hizo walipaswa kujadiliwa kwenye vikao rasmi,” alisema Mwankina.

Alisema Mbowe aliyefika hivi karibuni mkoani humo kusikiliza mgogoro huo, alipokea malalamiko ya kila upande, lakini hawakupaswa kuwavua madaraka ambayo waliyapata kwa kuchaguliwa.

Kauli za wajumbe hao zinatolewa wakati hali ya Chadema jijini hapa ikizidi kuwa tete kutokana na madiwani kuhasimiana

Mahiza Abaini Ufisadi Tanga..Sh36 Bilioni za Miradi 66 Zimetafunwa..Wapewa Siku 14

by


Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mwantumu Mahiza amesema Sh36 bilioni zilizotengwa kwa ajili ya kutekeleza miradi 66 ya ujenzi wa mabwawa ya umwagiliaji Tanga, zimefujwa.

Mahiza alisema hayo juzi katika kikao cha wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama, makandarasi, wahandisi na wakurugenzi wa wilaya za Mkoa wa Tanga.

Alisema ni miradi 30 tu iliyotekelezwa huku mingine 36 ikiwa haijatekelezwa na fedha kutumika.

Mahiza alifanya kikao hicho baada ya kumaliza ziara yake ya siku 10 ya kukagua miradi ya maji mkoani humo na kubaini ufisadi huo.

“Nawapa siku 14 mniletee maelezo kwa nini msichukuliwe hatua kwa kufanya kazi isiyo na tija na kuonyesha uchu wa kutaka fedha za miradi hali mkijua hamuwezi kuitekeleza na kutoishauri Serikali kuhusu njia sahihi,” alisema.

Alisema makandarasi na wahandisi ambao hawakutekeleza miradi watakuwa chini ya uchunguzi wa maofisa wa Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (Takukuru), Idara ya Usalama wa Taifa na Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).

“Sh36 bilioni zimehujumiwa na wataalamu (watendaji) ambao hawaitakii mema Tanga, imenigusa, imeniumiza kupita kiasi, nimekasirika, haya ni majipu makubwa tutayatumbua bila ganzi.

“Mmetutengenezea fitina kati ya Serikali na wananchi,” alisema Mahiza.

Alisema baada ya kupokea maelezo hayo atakutana na kamati yake ya ulinzi na usalama kushauriana kisha majina yote ya waliohusika yatafikishwa kwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kwa ajili ya uamuzi.

Mhandisi wa Maji Mkoa wa Tanga, Ephraim Minde alisema miradi hiyo 30 iliyokamilika ipo katika Wilaya za Korogwe, Lushoto, Kilindi na Tanga.

Mmoja wa wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Noel James alisema mradi wa umwagiliaji wa Mwakijembe Wilaya ya Mkinga unaofadhiliwa na Benki ya Dunia.

Halima Mdee Atupwa Rumande......Mahakama Yakana Kuzuia Uchaguzi wa Meya Dar es Salaam Wadai Agizo Lilikuwa Feki

by

Wakati mbunge wa Kawe (Chadema), Halima Mdee akilala rumande akihusishwa na vurugu zilizotokea Jumapili wakati uchaguzi wa meya wa Jiji la Dar es Salaam ulipokwama, Mahakama ya Kisutu imelikana zuio lililotumika kuzuia shughuli hizo.

Uchaguzi huo ulipangwa kufanyika Januari 23, mwaka huu, lakini uliahirishwa ili kuandaa mfumo bora wa upatikanaji wajumbe kutokana na CCM kutaka kuingiza wapigakura nje ya waliotakiwa.

Ulikwama tena Februari 8, baada ya Halmashauri ya Jiji la Dar kubaini kasoro ya nyongeza ya majina 14 ya wajumbe kutoka manispaa za Ilala na Kinondoni.

Jumapili iliyopita ilikuwa ni mara ya tatu, kukwama tena kutokana na zuio lililosababishwa na kesi iliyofungiliwa na Saad Kimji na Suzan Masawe.

Hata hivyo, zuio hilo la muda la Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu lililotumika kuahirisha uchaguzi wa meya na naibu meya wa Jiji, uliopaswa kufanyika Februari 27, 2016 limebainika kuwa ni batili.

Jana, Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Kisutu, Waliarwande Lema alisema Saad Kimji na Suzan Massawe walifungua kesi Februari 5, 2016 wakizuia uchaguzi wa meya na naibu wake ambao ulipaswa kufanyika Februari 8,2016.

Hakimu Lema alibainisha baada ya kufungua shauri hilo, Mahakama ya Kisutu iliweka zuio la muda ili kesi hiyo ianze kusikilizwa Februari 15, 2016 lakini walalamikaji hawakutokea mahakamani hivyo mahakama ikapanga kusikiliza kesi hiyo Februari 23, lakini hawakutokea pia.

Alisema kutokana na hali hiyo, aliliondoa shauri hilo mahakamani hapo na hivyo zuio hilo likawa limekufa.

Aliongeza kuwa aliyesema Mahakama ya Kisutu imetoa zuio ni muongo na kwamba zuio halali ni lazima liwe na jina la Hakimu pamoja na sahihi.

Kukamatwa kwa Mdee
Katika sakata la jana, Mdee na madiwani wengine watatu walilazwa rumande kutokana na kutuhumiwa kumshambulia Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es Salaam, Theresia Mmbando

Wanatuhumiwa kufanya kosa hilo baada ya vuta nikuvute kutokea Jumapili iliyopita wakati shughuli ya kuwasaka viongozi hao wa jiji zilipokwaa kisiki kwa mara ya tatu, na CCM kuamua kukimbilia mahakamani.

Hali hiyo, ilizua tafrani kati ya madiwani na wananchama wa vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) baada ya uchaguzi huo kuahirishwa kwa zuio la muda la Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Tafrani hiyo ndiyo iliyosababisha vurugu ambazo inadaiwa kuwa katika purukushani hizo Mdee alimshambulia Mmbando mara baada ya kutangaza kuahirisha uchaguzi huo.

Polisi waliokuwa wanalinda usalama kwenye ukumbi wa Karimjee ambako uchaguzi huo ulitakiwa kufanyika, walimtoa nje Mmbando.

Akitoa maelezo mafupi kwa waandishi wa habari jana baada ya Mdee kuhojiwa kwa takriban saa sita, wakili wake , Profesa Abdalah Safari alisema mbunge huyo anashikiliwa kwa kosa hilo na atalala rumande.

“Kimsingi nilikuja kumsikiliza akitoa maelezo yake, ameshatoa lakini hakuna ushahidi wowote wa kosa analodaiwa kufanya la kushambulia Theresia,” alisema.

Hata hiyo, Profesa Safari alisema kutokana na kosa hilo Mdee alikuwa na haki ya kuwekewa dhamana lakini polisi wamekataa.

“Mdee angeweza kujidhamini hata mwenyewe lakini wamekataa na kutokana na kosa hili anatakiwa kulala rumande kwa saa 48, zikizidi ina maana atapelekwa mahakamani,” alisema.

Profesa Safari, ambaye pia ni makamu mwenyekiti wa Chadema Bara, alisema mbali na Mdee pia madiwani watatu wanashikiliwa na polisi kwa kosa hilo.

Madiwani hao ni Humphrey Sambo wa kata ya Mbezi, Ephraim Kinyafu (Saranga), wakati hakumtaja jina diwani wa tatu.

Awali wakati mahojiano hayo yalipoanza saa 7:00 mchana, taarifa kutoka kwa mmoja wa makada wa chama hicho zilieleza kuwa Mbunge wa Ukonga (Chadema), Mwita Waitara pia alitakiwa kufika kituoni hapo kutoa maelezo na anatarajiwa kuwasili leo.

Wakati wa polisi wakimhoji Mdee, wanachama wa Chadema walifika kituoni hapo, akiwapo Ester Bulaya, ambaye ni mbunge wa Bunda Mjini, Esther Matiko (Bunga Vijijini) na Henry Kilewo ambaye ni kanda wa Chadema.

Mapema jana mchana kabla ya Mdee kufikishwa kituoni hapo, ilielezwa kuwa polisi walizingira nyumba yake na kumtaka aende kituoni.

Hata hivyo, mbunge huyo hakutoka hadi alipowasiliana na wakili wake ambaye alienda naye kituoni kwa ajili ya mahojiano.

January Makamba Aikosoa Serikali ya Jakaya Kikwete

by



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), January Makamba ametofautisha nyakati za utawala wa Serikali ya Awamu ya Nne iliyoongozwa na Dk. Jakaya Kikwete na zilizopita na huu wa Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais John Magufuli, huku akiitoa kasoro iliyopita.

Makamba ameeleza kuwa wakati tawala zilizopita, watu walikuwa wakionewa haya na na kujuana kulichukua nafasi tofauti na awamu hii inayochukua hatua stahiki bila kujali.

“Nadhani moja ya changamoto zilizosababisha huko nyuma tusifanikiwe sana katika suala la uwajibikaji, ni hili suala la kuoneana haya. Suala la kujuana kidogo na kusitiriana,” Makamba aliliambia Gazeti la Mwananchi hivi karibuni.

Alisema kuwa utamaduni huo unapoendelea na kuota mizizi, suala la uwajibikaji huwa kikwazo na hatua stahiki dhidi ya watu wanaofanya makosa hushindwa kuchukuliwa.

Makamba ambaye alikuwa Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia katika Serikali ya Awamu ya Nne, alieleza kuwa hatua za utumbuaji majipu zinazochukuliwa hivi sasa dhidi ya wakwepa kodi na watumishi wanaovunja sheria na kutowajibika ni sahihi na kwamba kama kuna mtu anaona anaonewa bado anayo nafasi ya kutafuta haki yake kwenye vyombo vya kisheria.

“Kikubwa tu ambacho mimi ninaamini ni kwamba kunahitajika kujenga utamaduni mpya wa watu kuogopa na kuheshimu wajibu wao, na kwamba hizi kazi si kazi zetu za kudumu. Wakati wote unapofanya makosa basi kuna Mamlaka ya kukuchukulia hatua,” alisema.

Makamba alisisitiza kuwa ni sahihi kuchukua hatua hivi sasa dhidi ya makosa yaliyofanyika katika utawala uliopita, “Kama huko nyuma hakukuwa na utashi wa mfumo wa kuwezesha makosa hayo kubainika, lakini utashi huo upo sasa, basi hatua zichukuliwe.”

Kaburi la Halaiki la Maiti zaidi ya 30..Lapatikana Burundi

by


Maafisa wa polisi na utawala wa mji mkuu wa Bujumbura Burundi wamegundua kaburi la halaiki linaloshukiwa kuwa na takriban miili 30.

Mwandishi wa BBC aliyeko huko Prime Ndikumagenge anasema kuwa miili 3 na fuvu la kichwa ilipatikana katika eneo la Mutakura Kaskazini mwa Bujumbura.

Kitongoji hicho cha Mutakura ni moja ya ile iliyosheheni wafuasi wa upinzani ambao walijitokeza mabarabarani wakiandamana kupinga kauli ya rais Pierre Nkurunziza kuwania muhula wa tatu uongozini.

Nkurunziza alitangaza nia ya kuwania muhula wa tatu mwezi Aprili mwaka uliopita kinyume cha katiba akidai kuwa mhula wa kwanza hakuchaguliwa na umma.

 Wapinzani wake hata hivyo wanadai kuwa alikiuka katiba ya taifa.

Meya wa mji wa Bujumbura Freddy Mbonimpa anasema walipokea habari hiyo kutoka kwa ''wahuni waliojisalimisha kwa utawala''.

Haikuelezwa kwa hakika waliuawa lini au na nani na nani aliyewazika pahala hapo.
Meya huyo hata hivyo alidai kuwa waliopatikana wameuawa walikuwa ni wafuasi wa rais Nkurunziza.

Kuwepo kwa makaburi ya halaiki kuligunduliwa kwanza na kundi linalopigania haki za kibinadamu la Amnesty International mwezi Januari.

Ripoti hiyo ya kundi la kutetea haki za binadamu la lilichapishwa tarehe 11 Desemba mwaka uliopita siku moja baada ya serikali kukiri kuwa wamewaua watu 79 na kupoteza maafisa 8 wa polisi.

Meya huyo leo amekiri kuwa utawala wake ulizika miili ya watu 58 katika makaburi ya halaiki katika makaburi yanayofahamika.

Umoja wa Mataifa unasisitiza kuwa zaidi ya watu 430 waliuawa nchini Burundi tangu kauli ya rais Nkurunziza kubainika mwezi Aprili.

HABARI Njema..Rufaa ya Babu Seya na Mwanaye Kuanza Kusikilizwa March 11 Mwaka Huu.

by

Mahakama ya Haki za Binadamu ya Afrika (AfCHPR) katika kikao chake kilichoanza jijini Arusha, itapitia maombi ya rufani ya mwanamuziki maarufu nchini, Nguza Viking na John Viking dhidi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Hata hivyo, taarifa iliyotolewa na mahakama hiyo jana, ilieleza kuwa kesi hiyo namba 006/2015 iliyopangwa kusikilizwa Machi 11 haitasikilizwa katika mahakama ya wazi.

Ni kesi mbili pekee kati ya 50 zitakazosikilizwa kwenye mahakama ya wazi, ikiwamo inayomhusu mwanasiasa maarufu wa Rwanda, Victoire Ingabire aliyoifungua kupinga ukiukwaji wa haki anaofanyiwa na Serikali yake.

Pia, mahakama ilieleza kuwa kikao hicho cha 40 cha kawaida kitakamilika Machi 18 na kutoa uamuzi wa mashauri manne.

Kesi ya Ingabire inayotarajiwa kuvuta hisia za watu wengi ikizingatiwa upinzani ambao amekuwa akiuonyesha dhidi ya serikali yake, itasikilizwa Machi 4.

Katika kesi hiyo, Ingabire pamoja na mambo mengine anadai haki zake kuvunjwa ambazo zinatajwa kwenye Mkataba wa Mahakama hiyo Ibara ya 7, 10 na 18 hivyo anaitaka itoe uamuzi.

Pia, Taasisi ya Action Pour la Protection des Droits de I’Homme (APDH) inaishtaki Serikali ya Ivory Coast kuvunja mkataba wa Mahakama ya Afrika na Haki za Binadamu Ibara ya 3 na 17 katika kesi namba 001/2014, iliyopangwa kusikilizwa Machi 3.

Mahakama hiyo inaundwa na majaji 11 kutoka nchi wanachama wa Umoja wa Afrika (AU) na inakuwa na vikao vinne kwa mwaka, kufikia Januari 31 tayari ilikuwa imepokea kesi 74 kati ya hizo 25 imetolewa uamuzi.

Maombi manne yamepelekwa  kwa uamuzi zaidi kwenye Kamisheni ya Afrika ya Haki za Binadamu.

Dudu Baya Awaita ‘Kenge’ Wanaosema Amefulia Adai yeye Bado ni Mamba

by

Dudubaya amewajia juu baadhi ya majirani zake na Watu wengine waliosema amefulia na amekuwa akishinda maskani muda wote kuvuta bangi.

Dudubaya amesema hao ni kenge wasioelewa maana ya maskani na daima atabaki kuwa mamba.

Maneno ya Dudubaya yamekuja siku chache baada ya baadhi ya majirani zake kupitia EATV kusema amefulia na anashinda maskani muda wote jambo ambalo jamaa amelikanusha vikali.

Amesema Watu lazima wajue siyo kila maskani ni mbaya.sometimes anakwenda maskani kubadilishana mawazo na washkaji na kupata ideas mpya za nyimbo akitoa mfano kuwa nyimbo nyingi zake zilizohit enzi hzo alipata idea zake maskani.kila MTU hata wanasiasa wana maskani,alisema Dudubaya

Umeya wa Dar Utamponza Magufuli...Bado Chama Chake Hakijawa na Dhamira ya Kweli ya Kutaka Mabadiliko

by

Siku chache baada ya Mhe.John Pombe Magufuli kuchaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na kuanza "kutumbua majipu" rafiki yangu mmoja ambaye ni mwandishi wa gazeti moja la kila siku aliniambia hii ni nguvu ya soda.

Alisema Magufuli anaweza kuwa na dhamiri ya kweli ya kufanya mabadiliko lakini atakwamishwa na chama chake. Bado chama chake hakijawa na dhamira ya kweli ya kutaka mabadiliko. Hata majipu anayotumbua kuna mengine hayatumbuliki maana yanagusa uhai wa chama chake.

Aliifananisha dhana ya "kutumbua majipu" na "kuvua gamba" ambayo ilitumika na chama cha mapinduzi miaka kadhaa iliyopita kama ajenda ya kupiga vita ufisadi. Lakini ajenda hii ilishindwa kuvua hata gamba moja ndani ya chama hicho licha ya kupigiwa chapuo na viongozi wakuu wa chama hicho.

Kwahiyo dhana ya "utumbuaji wa majipu" ni sawa na "uvuaji gamba". Kuna majipu hayawezi kutumbulika hata kama Rais Magufuli ana dhamira ya kufanya hivyo.

Moja ya jipu kubwa kabisa ambalo lipo usoni kwa Magufuli na amelikalia kimya kama hajaliona ni suala la umeya wa Jiji la Dar es Salaam. Hili ni jipu ambalo Magufuli ameshindwa kulitumbua na haoneshi kuwa na mpango huo.

Tangu uchaguzi mkuu ufanyike na wananchi kuchagua wabunge na madiwani yapata miezi minne sasa. Katika kipindi hiki cha miezi minne jiji la Dar es salaam ni kama limesimama.

Jiji halina Meya, hakuna kamati za halmashauri, hakuna mipango ya maendeleo, hakuna vikao vya madiwani, jiji limesimama kwa sababu ya mvutano wa kisiasa kati ya CCM na Muungano wa vyama vya UKAWA juu ya nafasi ya Umeya.

Mvutano huu umesababishwa na CCM kutokubali kuachia madaraka ya kuongoza jiji la Dar kwa vyama vya upinzani. Bado haijajulikana hofu ya CCM inatokana na nini lakini hadi sasa wamefanya mbinu mbalimbali kuhakikisha wanahujumu uchaguzi wa Umeya wa Dar na kuweza kuongoza tena jiji hili.

Baadhi ya mbinu zilizotumika ni pamoja na kutumia wabunge wa viti maalumu kutoka Zanzibar ambao baada ya mvutano mkubwa wa kisheria walizuiwa kupiga kura ya kumchagua Meya.

Lakini watu wanahoji kwanini CCM walete wabunge wa Zanzibar kuja kupiga kura Dar? CCM walijua kuwa wabunge wa Zanzibar hawana uhalali wa kisheria wa kupiga kura bara lakini wakalazimisha. Kwanini?

Baada ya wabunge hao kuzuiwa kushiriki uchaguzi huo CCM hawakuridhika. Wakabuni mbinu nyingine ya kuwatumia Mawaziri walioteuliwa kuwa wabunge kabla ya kuapishwa. Hilo nalo likakumbana na kizingiti cha kisheria.

Hatimaye uchaguzi ukaitishwa tena tarehe 05 mwezi February mwaka 2016 lakini Chama cha mapinduzi kikakimbilia Mahakamani kuweka zuio la kuahirisha uchaguzi huo. Kwahiyo wajumbe wakafika ukumbini na kutangaziwa kuwa uchaguzi huo umeahirishwa.

Hatimaye uchaguzi huo ukaitishwa tena kwa mara ya nne jumamosi ya tarehe 27 mwezi February mwaka huu.

Katika uchaguzo huo Theresia Mbando aliyekuwa Mwenyekiti wa Mkutano huo, aliwataka wajumbe wote kuingia ukimbini ili mkutano huo kuanza.

Baada ya wajumbe kuingia ndani, Mbando alifuata taratibu zote za kiitifaki katika kufungua kikao hicho ikiwa ni pamoja na kugawa ratiba za mkutano huo.

Wajumbe wakiwa tayari kwenda na ratiba ya mkutano huo, ndipo Bi.Sara Yohana (Kaimu Mkurugenzi wa jiji) alisimama ghafla na kutangaza kuhairishwa kikao hicho kwa madai kwamba, amepokea zuio kutoka Mahakama ya Kisutu iliyomtaka kutoendesha uchaguzi huo. Hali hiyo ilizua taharuki na kusababisha vurugu kubwa.


Katika maelezo yake kwa wajumbe Bi.Sarah alionesha nakala ya zuio la Mahakama ya Hakimu mkazi Kisutu iliyotolewa tarehe 5 mwezi February mwaka huu.


Watu wanahoji ikiwa kulikua na zuio la Mahakama kuanzia tarehe 5, kwanini Mkurugenzi aliitisha uchaguzi na kualika wajumbe? Kulikua na haja gani ya kujulisha umma kuwa uchaguzi upo na watu wakafika kumbe kuna zuio la mahakama?

CCM WANA HOFU GANI?
Kutokana na hali inayoendelea yapo maswali mengi yanayoibuka juu ya hofu ya CCM kwenye uchaguzi huu. Je kwanini CCM hawataki kuachia Halmashauri ya jiji iongozwe na upinzani? Wanahofia nini?

Baadhi ya wachambuzi wa masuala ya kisiasa wanasema CCM wana hofu mbili. Kwanza wanahofia kupoteza mamlaka ya kimaamuzi katika mambo yanayohusu maendeleo ya jiji la Dar.

Kwa kuwa jiji litaongozwa na upinzani, CCM watakosa nguvu ya kufanya maamuzi katika mipango ya maendeleo ya jiji, na hivyo watashindwa kutekeleza ilani yao. Hali hii itatoa fursa kwa vyama vya UKAWA kutumia nafasi hii kujiimarisha zaidi kimipango, mikakati na kuwa na mamlaka kuzidi CCM.

Ikumbukwe halmashauri ya jiji la Dar es Salaam ndiyo inayoongoza kwa makusanyo ya mapato kulinganisha na Halmashauri nyingine nchini. Halmashauri ya jiji la Dar inakadiriwa kukusanya jumla ya shilingi Bilioni 10.7 kwa mwezi, ambapo kati ya hizo Bil 6.9 ni mapato ya ndani na Bil 3.8 ni ruzuku ya serilali. Mapato haya ni makubwa kuliko maapato ya majiji yote yaliyosalia ukiyaweka kwa pamoja.

Pengine hii ndiyo hofu ya CCM. Kwamba wanahofia fedha hizi zitatumika kutekeleza miradi ya maendeleo chini ya utawala wa vyama vya upinzani na hivyo vyama hivi vitapata fursa ya kujiimarisha zaidi.

Lakini upo mtizamo mwingine kwamba hofu ya CCM sio juu ya yatakayofanyika bali juu ya yaliyofanyika. Hawahofii UKAWA watafanya nini wakiingia madarakani, wanahofia wao walifanya nini walipokua madarakani.


Kuna taarifa kuwa kuna uchafu mwingi katika Halmashauri ya jiji la Dar na CCM wanahofia UKAWA wakishinda uchaguzi wataweka wazi uchafu huo.

Yapo madai kuwa miradi mingi ya maendeleo ilitekelezwa chini ya kiwango kwa kuwa wakandarasi walilipwa pesa kidogo kulinganisha na bajeti iliyotengwa. Pesa nyingine zilifanyiwa ufujaji na watendaji wa halmashauri. Hivyo CCM wanahofia ikiwa UKAWA wataingia madarakani watawaumbua.

Mojawapo ya miradi yenue malalamiko mengi ni uuzwaji wa Shirika la la Usafiri Dar es Salaam (UDA) amabalo liliuzwa katika mazingira ya kutatanisha kwa kampuni ya Simon Group ya jijini Mwanza.


Tarehe Mei 24, 2011 Mkurugenzi mkuu wa Simon Group Ndugu Simon Kisena alimuandikia barua Katibu Mkuu Wizara ya Miundombinu akimjulisha kuwa hadi wakati huo yeye ndiye aliyekuwa mmiliki mkuu wa UDA, baada ya kununua hisa 7,880,303 sawa na asilimia 52.35 ya hisa zote za UDA kati ya hisa 15,000,000 za awali kwa gharama ya Sh milioni 285.

Lakini gazeti la Jamhuri la tarehe 26 January mwaka 2016 liliandika habari juu ya ukaguzi uliofanywa kwenye kampuni hiyo ya Simon group na kampuni ya ukaguzi ya Philip & Company ilionesha kuwa Kampuni ya Simon Group ilipata faida ya Bilioni 1.7 baada ya kufanya kazi mwezi mmoja tu tangu walipoinunua UDA.

Yani walinunua UDA kwa Milioni 285 lakini baada ya kufanya kazi kwa mwezi mmoja tu wakapata faida ya Bilioni 1.7. Hii ni faida kubwa sana na isiyotarajiwa katika mazingira ya kawaida.

Ikiwa UDA ilikua na uwezo wa kuingiza faida ya Bilioni 1.7 kwa mwezi kwanini iliuzwa kwa Milioni 285 tu? Bila shaka kuna mazingira ya ufisadi katika sakata la uuzwaji wa UDA. Wapo viongozi kadhaa ambao wamewahi kutuhumiwa kuwa walishiriki kuuza UDA kinyemela.

Huu ni mfano mmoja tu kati ya mifano mingi inayohusu uchafu uliofanyika katika halmashauri ya jiji la Dar wakati jiji likiongozwa na CCM. Na pengine uchafu wa aina hii ndio unaowapa hofu CCM kuachia halmashauri hii kuongozwa na vyama vya upinzani kwa vile wataumbuka.

Kama wameweza kuumbuka Ilala sembuse halmashauri ya jiji? Taarifa ya Meya wa Ilala Mhe.Charless Kwiyeko aliyoitoa mwishoni mwa wiki iliyopita inaonesha kuwa kuna ubadhirifu mkubwa ulifanyika katika halmashauri hiyo wakati ikiwa inaongozwa na CCM.

Mojawapo ni mishahara kwa mgambo wa jiji. Taarifa ya ukaguzi ilionesha kuwa Askari Mgambo wa jiji hulipwa kiasi cha shilingi 280,000/= kwa mwezi lakini malipo halisi waliyokua wakipata ni shilingi 60,000/= kwa mwezi.

Hii ina maana kwamba kila Askari Mgambo alikua akikatwa shilingi 220,0000/= katika mshahara wake ambapo alikua hajui zinapoenda. Huu ni ufisadi na unyonyaji wa kiwango kisichovumilika.

CCM WANA MPANGO GANI?
Hadi sasa CCM wametumia mbinu mbalimbali kuhakikisha wanaongoza halmashauri ya jiji la Dar lakini imeshindikana. Pamoja na kutumia madiwani kutoka Zanzibar na kuweka zuio mahakamani bado wana hofu ya kushindwa uchaguzi kwa kuwa wana idadi ndogo ya madiwani kulingamisha na wale wa UKAWA. CCM ina jumla ya madiwani 76 na UKAWA 87 hivyo inatarajiwa Uchaguzi ikifanyika CCM wataanguka.

Lakini pamoja na kuwa na idadi ndogo ya madiwani bado wana mpango wa kuongoza halmashauri ya jiji la Dar kwa kutumia mbinu yoyote. Kwa kuwa demokrasia inaonekana kushindwa kuwapa fursa ya kuongoza wanaweza kutumia mbinu nyingine zisizo za kidemokrasia.

Mbinu kubwa inayotarajiwa ni kama ile iliyotumika mwaka 1996. Tarehe 28 mwezi June mwaka 1996 aliyekuwa Waziri Mkuu Mhe.Fredrick Sumaye aliivunja Halmashauri ya jiji la Dar na kuunda Tume maalumu ya muda kwa ajili ya kuongoza jiji hilo kwa madai ya rushwa na jiji kukusanya mapato chini ya kiwango.

Sheria ya serikali za mitaa ya mwaka 1982 [Local Government Act (Urban Authorities) of 1982] pamoja na sheria nyinginezo zinazosimamia serikali za mitaa na majiji zinampa Waziri Mkuu mamlaka ya kuvunja halmashauri ya jiji/mji/manispaa na kuteua Tume ya muda ya kuongoza eneo hilo.

Lakini ili kufanya hivyo ni lazima kuwepo na sababu ya kumfanya Waziri Mkuu kufanya maamuzi hayo. Mwaka 1996 Sumaye aliivunja halmashauri ya jiji kwa kuwa alikua na sababu. Hakuivunja tu kienyeji. Na sabu zenyewe ni mbili. Moja ni madai ya rushwa na pili ni kukusanya mapato chini ya kiwango.

Lakini mwaka huu Waziri Mkuu hana sababu ya kumfanya aamue hivyo. Kama ni mapato, jiji la Dar wanakusanya zaidi ya matarajio. Mwaka 2014/15 walipanga kukusanya Bilioni 10.1 kwa mwaka lakini wakakusanya wastani wa Bilioni 10.7 (zidio la milioni 600).

Kwa hiyo Waziri Mkuu hana sababu ya kuivunja Halmashauri ya jiji lakini CCM wanataka kumpa sababu.

Kitendo cha kuitisha uchaguzi huku wakijua wazi kwamba kuna zuio la Mahakama inaonekana ni mpango wa kuwakasirisha wafuasi wa UKAWA waliokua wamefurika ukumbini ili wafanye fujo na Waziri mkuu atumie fujo hizo kama kigezo cha kuvunja halmashauri ya jiji na kuunda Tume ya muda kuongoza.


Kwa kufanya hivyo atakua amefanikiwa kuhujumu haki ya UKAWA kuongoza jiji la Dar na kuwapa fursa CCM kubaki madarakani kupitia mlango wa uani wa kuunda Tume.

RAIS MAGUFULI ANA NAFASI GANI KATIKA HILI?
Watu wengi wanajiuliza kwanini Rais Magufuli amekaa kimya juu ya suala hili kwa takribani miezi minne sasa. Magufuli ambaye amejitanabaisha kuwa muadilifu kwanini hachukui hatua zozote juu ya swala hili. Kitendo cha kukaa kimya huku akishuhudia demokrasia ikibakwa kinatilia mashaka uadilifu wake.

Hali hii inafanya watu wafike mbali zaidi na kuhoji juu ya ushindi wake. Ikiwa CCM hawako tayari kushindwa katika ngazi ya halmashauri ya jiji, je wangeshindwa katika uchaguzi mkuu nafasi ya Rais wangekubali.?

Ikiwa jambo dogo kama la umeya wamekataa kuheshimu demokrasia, je wanaweza kuheshimu demokrasia katika Uchaguzi ngazi ya kitaifa?

Kwanini Rais Magufuli anatumbua majipu yaliyojificha lakini jipu la Umeya Dar analilea? Kwanini asiwashauri CCM waheshimu demokrasia na maamuzi ya Wananchi?

Miezi minne sasa jiji la Dar es Salaam limesimama. Hakuna mipango ya maendeleo, hakuna vikao vya halmashauri kwa sababu ya CCM kukataa kuheshimu demokrasia. Je Magufuli anaona hili ni sawa?

Kwamba watu waendelee kuteseka kwa kukosa huduma, mipango ya maendeleo isipangwe, kwa sababu tu CCM hawako tayari kushindwa? Je hii ni sawa?

Kitendo cha Rais Magufuli kukaa kimya kwenye suala hili kinamfanya aonekane hana dhamira ya kweli ya kuleta mabadiliko. Hana tofauti na watangulizi wake. Anakipenda zaidi chama chake kuliko anavyowapenda watanzania. Ndio maana yuko tayari kuona chama chake kikivunja demokrasia na wananchi wakiteseka lakini akakaa kimya, kwa sababu tu uvunjaji huo wa demokrasia unakinufaisha chama chake.

Hili ni doa katika utendaji wake, na asipochukua hatua za dharura atapoteza imani yake aliyoanza kuijenga mbele ya jamii ya Watanzania.

Chanzo :Malisa Godlisten

Bunge la Afrika Mashariki Lampongeza Rais Magufuli Kwa Hapa Kazi tu

by

Bunge la Afrika Mashariki limempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa kazi nzuri anayoifanya ya kuhakikisha mapato ya nchi yanakusanywa kikamilifu na yanawanufaisha wananchi wote.

Akiongea kwa niaba ya wabunge hao mbunge Shyrose Bhanji amesema kuwa eneo kubwa ambalo Rais amehakikisha linasimamiwa vizuri ni eneo la bandari eneo ambalo limerudisha heshima na uaminifu kwa wafanyabiashara kutumia bandari ya Tanzania na hivyo kuongeza mapato ya nchi.

Mheshimiwa Banji ameongeza kuwa nchi zote za Afrika Mashariki zinaitegemea sana bandari ya Dar es salaam hivyo nchi wanachama wa Afrika Mashariki wamekuwa na furaha kubwa kuona kuwa bandari hiyo imepiga hatua na wana uhakika kuwa bandari hiyo itarahisisha biashara kwa wafanyabiashara wa ukanda huo.

Sina Mpango wa Kuoa Mtu - Ney wa Mitego Afunguka..

by

Msanii Ney wa Mitego amesema kwa sasa hana mpango wa kuoa na wala hafikirii kuoa, licha ya kuwa na watoto ambao wanahitaji malezi ya mama.

Ney ameyasema hayo kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio, na kusema kwa sasa hayuko kwenye mahusiano yoyote, na suala la kuoa kwake ni suala zito, hivyo hawezi kukurupuka na kuchukua uamuzi wa kuoa.

"Kusema kweli kabisa nimeulizwa swali ambalo sijaulizwa muda mrefu, na nikiulizwa huwa nalikwepaga, kufuatana na mahusiano ambayo nimekuwa nayo katikati, namshukuru Mwenyezi Mungu amenijalia watoto, for this time nikisema nizungumzie kuhusu ndoa nitadanganya, mi sifikirrii kabisa kuhusu kuoa for this time, kwa bahati mbaya au mzuri mi sipo kwenye mahusiano, sitaki kukurupuka, unajua ukifunga ndoa kwa sisi, mi ni mkristo hiyo ndo nitolee, yani hapo ndo umejicomit umeshaingia kwenye 18 ambazo huwezi kuzipangua tena, sifikirii kuoa, siwazi na sidhani kama nina huo mpango", alisema Ney wa Mitego.

Pamoja na hayo Ney wa Mitego amekiri kuwa na mahusiano na Mtanzania Stella a.ka Chaga Baby ambaye anaishi Marekani, lakini umbali uliopo kati yao ndio chanzo cha wao kutokuwa pamoja.
"
Chaga baby ye yuko mbali kiukweli kabisa, labda kitu ambacho sijawahi kuzungumza kwanza kiukweli kabisa, mi nipo huku, alafu bado ana ratiba ndefu ya kuendelea kuwa kule, mi nimwanaume sitaki kuoneka mwanaume muongo ambaye anajipa matumaini ambayo hayana kichwa wala miguu, lakini wakati ukifika kama atakuja au mi nitaenda kila kitu kitakuwa sawa, but for this time niko single", alisema Nay wa Mitego

Nay wa Mitego Adai Hela Pamoja na Mali Anazomiliki Zina Thamani ya Bilioni Moja

by

Nay wa Mitego Akiwa na Gari yake
Staa wa muziki Nay wa Mitego amedai kuwa hela anazomiliki benki pamoja na mali anazomiliki zina thamani ya bilioni 1.

Akizungumza katika kipindi cha Weekend Chat Show cha Clouds TV Ijumaa hii, Nay alisema biashara pamoja na muziki wake ni vitu vinavyomwingizia pesa nyingi.

“Mimi mali zangu na kila kitu zinafika kwenye bilioni hivi, ukichanganya hela zilizo benki pamoja na biashara ninazofanya thamani yake zinafikia bilioni moja na kitu. Sitaki kudanganya watu sijui kwenye bilioni 2 huko,” alisema Nay.


Nay alisema hela hizo amezipata kupitia biashara ya daladala pamoja na muziki wake.

Rapa huyo mwaka 2014 alihamia kwenye nyumba yake iliyopo Mbezi jijini Dar na kudai nyumba hiyo ina thamani ya milioni 200.

Top Ad 728x90